Kikao cha kwanza cha Shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi UN-Habitat kinaendelea mjini Nairobi, Kenya, kikiwa na kauli mbiu ya "uvumbuzi kwa ajili ya maisha bora mijini na maeneo ya makazi". Akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano huo jana, mkurugenzi mtendaji wa UN-Habitat Maimunah Mohd Sharif alisema asilimia 70 ya watu duniani wanatarajiwa kuishi mijini ifikapo mwaka 2050, jambo litakalotoa changamoto kwa kila nchi katika kutoa huduma za kimsingi kama vile nyumba, usafiri, nishati, ajira, elimu na huduma za matibabu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |