Shirika la Utangazaji la Japan NHK limeripoti kuwa jumla ya watu 20 wamejeruhiwa kwa kuchomwa kisu, watatu wakiwa mahututi baada ya kushambuliwa na mwanamume mmoja katika bustani moja huko Kawasaki, karibu na Tokyo. Kati ya watu hao 20, 16 ni watoto wa shule ya chekechea. Mtuhumiwa huyo aliyejeruhiwa vibaya begani anashikiliwa na polisi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |