Kutokana na waziri mkuu wa Israel Bw. Benjamin Netanyahu kushindwa kuunda baraza la mawaziri kama ilivyopangwa, bunge la nchi hiyo jana limepiga kura na kupitisha mswada uliotolewa na chama cha Likud kinachoongozwa na Bw. Netanyahu kuhusu kuvunja bunge la 21 na kuitisha uchaguzi mpya.
Kutokana na kushindwa kufikia makubaliano na kiongozi wa chama cha Israel Beiteinu Bw. Avigdor Lieberman kuhusu kuunda muungano wa utawala, Bw. Netanyahu hakuweza kuunda baraza lake la mawaziri kabla ya tarehe 29, mwezi wa Mei. Habari zinasema, uchaguzi mpya wa bunge utafanyika tarehe 17 Septemba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |