Waziri mkuu wa India Narendra Modi ameapishwa kwa muhula wake wa pili katika sherehe zilizohudhuriwa na rais Ram Nath Kovind zilizofanyika Ikulu. Zaidi ya mawaziri 45 pia wameapishwa baada ya Modi. Waziri mkuu wa China Li Keqiang amempongeza Modi kwa kuchaguliwa tena, na kueleza matumaini yake ya kuendelea na ushirikiano wao ili kukuza zaidi uhusiano wa kiwenzi kati ya nchi zao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |