Msikiti wa Al-Azhar wa Misri ambao ni msikiti mkuu wa dhehebu la Sunni duniani pamoja na makanisa ya Orthodox na Katoliki nchini humo yamelaani vikali shambulizi la kigaidi lililotokea jimboni Sinai Kaskazini jana katika sikukuu ya Eid al-Fitr. Shambulizi hilo lililofanywa dhidi ya kituo cha ukaguzi mjini Arish limesababisha vifo vya askari 8 wa usalama, huku magaidi 6 wakiuawa katika mapigano. Wakati huohuo baadhi ya nchi za kiarabu ikiwemo Bahrain, Kuwait and Jordan pia zimelaani shambulizi hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |