Kaimu mrajisi wa Bodi ya maziwa Tanzania TDB Bi. Sophia Mlote amesema viwanda 15 vipya vya maziwa vimeanzishwa nchini humo baada ya serikali kuu kuamua kudhibiti uingizaji ovyo wa bidhaa za maziwa.
Ofisa huyo amesema viwanda hivyo vina uwezo wa kuchakata lita 90,400 za maziwa kwa siku.
Mwaka jana, wizara ya mifugo na uvuvi ya Tanzania ilizindua operesheni maalumu ya kudhibiti uingizaji ovyo wa bidhaa za maziwa, ambazo zimevuruga soko la ndani nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |