Msemaji wa mkoa wa Herat wa Afghanistan Bw. Jailani Farhad amesema, wapiganaji 38 wanaohusiana na kundi la Taliban wameachiliwa huru kutoka jela mkoani humo.
Rais wa Afghanistan alitangaza kuachilia wafungwa 900 wiki iliyopita, ikiwa ni ishara nzuri ya kuwahamasisha wapiganaji wa Taliban kufanya mazungumzo na serikali ili kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wa nchi hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |