• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Coca Cola kuwekeza shilingi bilioni 5 kuregeleza taka

    (GMT+08:00) 2019-06-11 19:33:18

    Kampuni ya Coca Cola itatumia shilingi bilioni 3.8 kwenye mradi wake wa kukusanya na kuregeleza chupa za plastiki kkatika maeneo ya mashahriki na kusini mwa Afrika.

    Kampuni hiyo imesema mradi huo unalega kufikia lengo la kuwa na dunia isiokwua na taka na kwamba inalenga kukusanya chupa zote kwenye maeneo ya takataka au zilzizotupwa ovyo.

    Rais wa Coca Cola kanda ya kusini na mashariki mwa afrika Bruno Pietracci amesema chupa zote zitakazokusanywa zitaregelezwa hapa hapa Afrika.

    Amesema pia kampuni nyingine ambazo hupakia bidhaa zao kwenye chupa za plastiki zimejiunga na kampeni hiyo.

    Tangu Januari Coca Cola na washirika wake wametoa dola milioni 5 kusaidia uregelezaji wa chupa za plastiki nchini Kenya, Mozambique, Namibia, Afrika Kusini, Tanzania, Uganda, Zambia na Zimbabwe.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako