Zaidi ya wanaridha 3,000 wamejiandikisha kushiriki mashindano ya 15 mbio za amani za Kigali. Kwa mujibu wa shirikisho la riadha la Rwanda limesema, zaidi ya wanariadha 1,000 waliojiandikisha ni wa mataifa ya nje na wanariadha zaidi wanatarajiwa kuendelea kujiandisha huku mwisho wa kujiandikisha ni Jumamosi Juni 16.
Mbio hizo zitakuwa mbio ndefu za kilomita 42.195, mbio fupi za kilomita 21, na mbio kwa ajili ya amani za kilomita 10 zitafanyika uwanja wa taifa wa Amahoro jijini Kigali Rwanda.
Mwanariadha mkongwe wa Ethiopia Drartu Tulu ambaye alikuwa mwafrika wa kwanza mwanamke kushinda medali ya dhahabu katika Olimpiki amethibitisha kushiriki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |