• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania kutangaza utalii China

    (GMT+08:00) 2019-06-13 19:39:40
    Bodi yaUtalii ya Tanzania (TTB) imejipanga kufanya ziara ya utangazaji wa utalii China ikiwa ni hatua ya kuhakikisha inavuna watalii kutoka nchini humo, hivyo kujiimarisha katika soko la utalii.

    Mwenyekiti wa Bodi ya TTB, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo, ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, ambapo alibainisha kuwa kiongozi wa msafara atakuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk. Aloyce Nzuki.

    Alisema ziara hiyo ya wiki moja inaanza Juni 19 hadi 26 katika miji minne ya China ambayo ni Beijing, Shangha, Nanjig, Changsha, lengo likiwa ni kuhakikisha Tanzania inaongeza sehemu ya umiliki wa soko kwenye soko la utalii China.

    Alisema katika ziara hiyo TTB itaambatana na wadau mbalimbali kutoka sekta binafsi na ya umma ikiwamo TANAPA, NCAA, Wakala wa Huduma za Misitu, Makumbusho ya Taifa Idara ya Mambo ya Kale Mamlaka ya Usimamizi wa wanyamapori na Wizara ya Maliasili na Utalii.

    Jaji Mihayo alisema Shirika la Utalii Dunia (UNWTO) na vyanzo vingine mbalimbali duniani vimebainisha kuwa soko la watalii kutoka China linaendelea kuongoza kwa kuwa na idadi kubwa zaidi ya watalii na mchango katika uchumi wa dunia.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako