• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa China atuma barua ya pongezi kwa mkutano wa Jukwaa la Maendeleo ya Tibet

    (GMT+08:00) 2019-06-14 20:44:41

    Rais Xi Jinping wa China ametuma barua ya pongezi kwa mkutano wa mwaka 2019 wa Jukwaa la Maendeleo ya Tibet uliofunguliwa leo katika mji mkuu wa mkoa huo, Lhasa.

    Katika barua hiyo, rais Xi amesema Tibet ni eneo muhimu la mpaka likiwa na makabila madogo, eneo muhimu la usalama wa kiikolojia,na pia sehemu muhimu ya ulinzi wa utamaduni wa kipekee wa taifa la China na pia kituo muhimu cha utalii.

    Ameeleza matumaini yake kuwa Tibet itachukua fursa kutokana na maendeleo, kuutangaza utamaduni wake wa kipekee, kulinda mazingira ya kiikolojia, kutekeleza kihalisi sera ya kufungua mlango, na kutoa sura mpya ya maendeleo ya Tibet katika zama mpya.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako