Aliyekuwa kocha wa timu ya taifa ya Hispania, Luis Enrique ameamua kung'atuka yeye na msaidizi wake huku akitoa sababu za matatizo ya kifamilia. Rais wa shirikisho la soka nchini Hispania (RFEF), Luis Rubiales siku ya Jumanne alifanya mabadiliko ndani ya timu hiyo. Luis Enrique aliukosa mchezo dhidi ya Malta mwezi Machi pamoja na San Marino, Sweden mwezi huu. Kocha namba mbili, Robert Moreno ndiyo amechukua nafasi yake. Vyombo vya habari za michezo nchini Hispania vinalazimika kumpa heshima yake, Luis Enrique kutokana na alichokifanya tangu alipoteuliwa ndani ya timu ya taifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |