• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • RIADHA: Wakenya Fancy Chemutai na David Bett wafanya tena mauaji kwenye mbio za kilomita 10 za Boston

    (GMT+08:00) 2019-06-25 08:35:01

    Wakenya Fancy Chemutai na David Bett wameibuka mabingwa wa mbio za kilomita 10 za Boston (B.A.A. 10k) nchini Marekani mnamo Juni 23, 2019. Chemutai na Bett, ambao wamejizolea Sh1 milioni kila mmoja, wamekata utepe kwa kukamilisha umbali huo kwa dakika 30:36 na 28:08, mtawalia. Chemutai alivunja rekodi ya B.A.A. 10k iliyowekwa na Mmarekani Shalane Flanagan mwaka 2016 kwa sekunde 16. Chemutai, ambaye ni mkimbiaji aliye na kasi ya tatu-bora duniani katika kilomita 10, alifuatwa kwa karibu na Wakenya wenzake Brilliant Kipkoech (31:04) na Caroline Rotich (31:58). Katika kitengo cha wanaume, Bett alifuatwa sekunde moja nyuma na Mkenya Daneil Chebii, huku Mkenya mwingine Stephen Sambu akifunga mduara wa tatu-bora kwa dakika 28:11.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako