Kampuni ya kusafirisha vifurushi ya Marekani FedEx imeifungulia mashtaka wizara ya biashara ya Marekani kuhusiana agizo la kuitaka kampuni hiyo iweke vizuizi dhidi ya kampuni ya Huawei.
Wizara ya biashara ya Marekani ilifikia uamuzi huo baada ya rais Donald Trump kutoa agizo la dharura kwa kile alichokiita hatari kwa teknolojia za Marekani.
Kwenye mashtaka hayo yaliyofunguliwa kwenye mahakama katika wilaya ya Columbia, kampuni ya FedEx inasema hatua ya wizara hiyo inaweka mzigo usio wa lazima kwa kampuni ya FedEx kukagua mamilioni ya vifurushi kwenye mtandao wake kila siku. Kampuni hiyo imesema serikali ya Marekani imetoa agizo ambalo linakiuka haki za kikatiba za kampuni hiyo, na ambalo ni vigumu kutekeleza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |