Wizara ya uchukuzi nchini Uganda imesema kuwa inatarajia kupokea ndege ya tatu aina ya CRJ-900 bombardier.
Waziri wa wizara hiyo Monica Azuba amesema ndege ya nne itawasili mwezi Septemba.
Ndege hizo mbili ni sehemu ya ndege 4 ambazo serikali ya Uganda iliagiza kutoka Canada ambako zinatengenezwa.
Ndege za kwanza mbili zilizonunuliwa kwa gharama ya dola milioni 41 ziliwasili Aprili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |