Aliyekuwa kiungo wa klabu ya Simba ya Tanzania raia wa Ghana, James Kotei amesaini mkataba wa miaka mitatu wa kuichezea klabu ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini.
Akizungumza sakata la kuondoka Simba, kiungo huyo bora wa mwaka wa Simba amesema kabla ya mkataba wake kuisha alikuwa akiwakumbusha viongozi wa klabu hiyo kwakuwa alikuwa amepata ofa toka vilabu mbalimbali wakati akiendelea kusubiri maamuzi yao, lakini viongozi hao hawakuonyesha nia ya kutaka kuendelea nae na kuamua kusaini klabu hiyo ya Afrika Kusini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |