Kasaija amesema hayo baada ya kurejea kutoka ziarani nchini China ambapo alihakikishiwa na serikali ya China kuwa ufadhili wa reli ya kisasa utatolewa pindi tu Kenya na Uganda zitakapomaliza mazungumzo.
Kenya inatarajiwa kujenga reli yake hadi eneo la mpakani la Malaba ili kuungana na Uganda.
Waziri kasaija pia amesema rais Yoweri Museveni, waziri wa uchukuzi wa Kenya James Macharia na waziri wa biashara wa China pamoja na maafisa wa benki ya EXIM ya china walifanya mkutano mjini Beijing kujadili hali ya baadaye ya kutolewa kwa ufadhili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |