Waasi wa kundi la Houthi la Yemen wamesema wamefanya mashambulizi 26 dhidi ya maeneo ya kijeshi katika viwanja vya ndege vya Saudi Arabia katika miezi miwili iliyopita. Taarifa iliyotolewa na msemaji wa jeshi la Houthi Yahya Sarea amesema mashambulizi 21 yalifanywa na ndege zisizo na rubani na mengine matano na makombora. Sarea ameongeza kuwa kundi hilo limetoa wito kwa raia kukaa mbali na vituo vya kijeshi vya Saudi Araibia na litaendelea na mashambulizi mpaka uvamizi dhidi ya nchi yao utakaposimamishwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |