Jumamosi Julai 6, Nigeria watakutana na Cameroon huku wenyeji Misri watakutana na Afrika Kusini. Na Jumapili Julai 7, Madagascar watawavaa DR Congo, nao Algeria watatoshana nguvu na Guinea. Na jumatatu Mali wao watacheza na Ivory Coast, huku Ghana uso kwa uso na Tunisia.
Mbali na timu zilizofuzu kutokana na kushinda mechi zao, timu nne pia zimefuzu katika raundi ya mtoano kama timu bora kati ya wale walioshindwa. Mataifa hayo ni Guinea, DR Congo, Afrika Kusini na Benin.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |