Kampuni ya Boeing imetangaza kutoa dola za kimarekani milioni 100 ili kushughulikia mahitaji ya familia za wahanga wa ajali mbili za ndege aina ya Boeing 737 Max 8 zilizotokea nchini Indonesia na Ethiopia mwezi Oktoba mwaka jana na mwezi Machi mwaka huu. Mkuu wa Boeing Dennis Muilenburg amesema kampuni yake itashirikiana na serikali za nchi hizo na mashirika yasiyo ya kiserikali kutoa pesa hizo katika miaka kadhaa ijayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |