Lengo la mfuko huo ni kushughulikia masuala ya fidia kwa wafanyikazi waliopo katika sekta rasmi ya umma na binafsi Tanzania Bara, ambao hupata matatizo ya kuumia, kuugua au kufariki kutokana na kazi wanazozifanya kwa mujibu wa mikataba hiyo. Kufikia sasa asilimia 85 ya waajiri wakubwa wamejisajili na mfuko huo, huku waajiri wadogo waliojisajili wakiwa asilimia 75.
Mfuko wa Fidia kwa Wafanyikazi ni taasisi ya hifadhi ya jamii iliyoundwa kwa mujibu wa sheria,kifungu cha 5 cha sheria ya Fidia kwa Wafanyikazi, sura ya 263, marejeo ya mwaka wa 2015, na kwamba kujisajili ni muhimu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |