• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Serikali yaonya wanaotoa mikopo ya pesa kwa njia ya simu

    (GMT+08:00) 2019-07-11 18:43:47
    Kampuni za kutoa mikopo ya pesa kwa kutumia maombi ya simu, huenda yakafanyiwa uchunguzi na kukaguliwa. Haya ni kwa mujibu wa Gavana wa Benki kuu ya Kenya Patrick Njoroge.

    Kulingana na Njoroge, kampuni hizi huenda zinatoa fursa na kuwachochea walaghai kusambaza pesa ghushi kwa wananchi. Gavana wa Benki kuu alitoa mfano wa mashirika ya Tala, Branch na Okash ambayo yanatumiwa sana na wakenya kukopa pesa, huenda yakatumiwa vibaya na walaghai kusambaza pesa ghushi. Mkuu huyo amesema kwamba lengo kuu la kukagua kampuni hizi ni kubaini wapi zinatoa pesa hizi za kuwapa wananchi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako