• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Tz na Uholanzi zaingia mkataba

    (GMT+08:00) 2019-07-11 18:46:53
    Serikali ya Tanzania na Uholanzi zimesaini makubaliano ya miaka mitano ya kusaidia kuinua maendeleo na ukuaji wa sekta za mifugo na uvuvi nchini. Makubaliano hayo yaliyosainiwa jana jijini Arusha yana lengo la kuona sekta za ufugaji kuku na samaki zinapata mwamko stahiki kwenye mifugo na uvuvi kwa kuwajengea uwezo Watanzania wa kujikita katika uchumi wa kati na viwanda ifikapo mwaka 2025.

    Akizungumza baada ya kusainiwa kwa makubaliano hayo, Naibu Waziri wa Kilimo na Ubora wa Chakula wa Uholanzi, Marjolijn Sonnema, alisema mpango huo utafanikishwa kupitia maofisa ugani nchi nzima. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega, alisema mkataba huo una maana kubwa kwa Tanzania kama nchi kwani utaongeza uzalishaji na kuinua maisha ya mfugaji. Alisema Tanzania inavuna kiasi cha tani 350,000 za samaki kwa mwaka ukilinganisha na mahitaji halisi ya tani 700,000.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako