• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Warwanda waanza kukimbilia fursa za biashara China

    (GMT+08:00) 2019-07-12 19:10:17

    Raia wengi wa Rwanda wameanza kukimbilia fursa za biashara nchini China.Baadhi ya bidhaa ambazo Warwanda wanasafirisha China ni pamoja na kahawa, chai, vinyago, pilipili na vinywaji. Mafanikio haya yametokana na ushirikiano mzuri uliopo kati ya China na Rwanda tangu waanze kutilia mkazo utengenezaji wa bidhaa za Rwanda.

    Rwanda imekuwa ikijihusisha na miradi mingi ya ushirikiano na China kama vile baraza la ushirikiano kati ya China na Afrika. Juni mwaka huu, China iliandaa shughuli nyingi tu za ushirikiano kati yake na Afrika katika miji ya Beijing na mkoa wa Hunan kupiga jeki sera yake ya kunufaishana katika mambo ya biashara na uchumi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako