Waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang ameitisha Kongamano la wataalamu wa uchumi na wanaviwanda, akichambua hali ya uchumi wa China kwa hivi sasa na kusikiliza maoni na mapendekezo kuhusu kazi ya uchumi katika kipindi kijacho.
Katika kongamano hilo, Bw. Li amesisitiza umuhimu wa kutekeleza mageuzi na ufunguaji mlango kwa hatua madhubuti, kuboresha muundo wa uchumi, kudumisha uendeshaji wa uchumi kwa utulivu ili kuhimiza uchumi kupata maendeleo yenye sifa bora.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |