Shirika la Biashara Duniani (WTO) limesema kuwa kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Bodi ya Rufaa ya Shirika hilo, hatua za kupinga utoaji ruzuku kwa bidhaa za China zilizochukuliwa na Marekani haziendani na sheria za Shirika hilo.
Ikiunga mkono matokeo ya jopo la usuluhishi wa mivutano la WTO yaliyotolewa March mwaka jana, Bodi hiyo imeamua kuwa, Marekani ilikwenda kinyume na makubaliano ya kupinga ruzuku katika hatua 11 za mchakato wake huu wa suala hilo.
Mwaka 2012, China iliwasilisha kesi za mshtaka katika WTO baada ya Marekani kutoza ushuru wa kupinga utoaji ruzuku dhidi ya bidhaa za China zilizouzwa nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |