Nusu ya watu wote waishio Afrika kusini mwa Sahara wanatarajiwa kutumia simu za mkononi ifikapo mwaka 2025. Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa Jumanne mjini Kigali, Rwanda na Muungano wa Mashirika ya Simu za Mkononi Ulimwenguni GSMA, kanda ya Afrika, kusini mwa Sahara, itaendelea kuwa na ongezeko la kasi zaidi la watumiaji wa simu za mkononi ambalo ni asilimia 4.6 kwa wastani kwa mwaka hadi mwaka 2025. Ripoti hiyo pia imesema Nigeria na Ethiopia zitashuhudia ukuaji wa kasi zaidi kuanzia sasa hadi mwaka 2025 kwa asilimia 19 na asilimia 11.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |