Mkuu wa Muungano wa upinzani wa Uhuru na Mabadiliko nchini Sudan Bw. Munzir Abul-Mali amesema, mkutano kati ya muungano huo na Baraza la Mpito la Kijeshi la Sudan, TMC kuhusu azimio la kikatiba uliopangwa kufanyika leo umeahirishwa kwa muda usiojulikana. Hata hivyo, hakutoa sababu za kuahirishwa tena kwa mkutano.
Jumatano wiki hii, pande hizo mbili zilisaini muswada wa azimio hilo la kisiasa, ikiwa ni hatua ya kufikia makubaliano na kujenga mfumo wa kipindi cha mpito.
Pande hizo mbili pia zilikubaliana kuahirisha kusainiwa kwa azimio la kikatiba, ambalo linaelekeza utaratibu wa mgawanyo wa madaraka katika kipindi hicho.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |