Kocha wa mbweha wa jangwani Algeria Djamel Belmadi na Kocha wa Simba wa Teranga ya Senegal Aliou Cisse wote walikuwa wachezaji wa kiungo na waliwahi kuchezea klabu za Uingereza katika ligi kuu ya EPL.
Mara ya mwisho kukutanisha makocha wazawa ilikuwa mwaka 1998 wakati Misri iliyokuwa ikifundishwa na kocha Mahmoud el Gohary ilikutana na Afrika Kusini iliyokuwa chini ya kocha Ephraim Sono.
Waswahili wanasema mtoto hatumwi dukani leo, nani kuibuka na ubingwa? Wadau wa soka wamegawanyika wengine wanarusha karata yao kwa Senegal wengine kwa Algeria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |