Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) limetoa ripoti ikisema ongezeko la uchumi katika mwaka 2019 na 2020 linakadiriwa kuwa asilimia 3.2 na 3.5, kiasi ambacho kimepungua kwa asilimia 0.1 kuliko makadirio yaliyotolewa mwezi April na Shirika hilo.
Ripoti hiyo imesema hakuna msukumo mkubwa kwa ukuaji wa uchumi duniani. Hadi sasa pato la ndani GDP na kiwango cha mfumuko wa bei zilizotangazwa na makundi mbalimbali ya kiuchumi zimeonesha kuwa, hali ya uchumi duniani haikui kama ilivyotarajiwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |