Wachezaji walioondolewa katika kikosi kutokana na kuwa majeruhi ni David Mwantika, Aishi Manula na Ibrahim Ajibu ambao nafasi zao zimezibwa na Haruna Shamte pamoja na Mohamed Ally Yusuf wote wa Lipuli na Oscar Godfrey Masai wa Azam FC.
Stars itamenyana na timu ya taifa ya Kenya (Harambee Stars) jijini Nairobi Agosti 4 kwenye mchezo wa marudio wa kufuzu michuano ya Chan inayotarajiwa kufanyika Cameroon 2020.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |