Waziri mkuu wa Palestina Bw. Mohammad Ishtaye ameilaumu Israel kwa kujaribu kuwafukuza raia wa Palestina kutoka Jerusalem. Bw. Ishtaye ametoa hoja hiyo katika mkutano uliofanyika huko Ramallah na wakazi wa Wad el-Hommos huko Sur Baher, kusini mashariki mwa Jerusalem, ambako serikali ya Israel iliharibu nyumba zao wiki mbili zilizopita. Bw. Ishtaye amesema, kilichotokea huko Wad el-Hommos ni uhalifu mbaya ambao haukubaliki, huku akiongeza kuwa Israel inajaribu kuwafukuza watu wa Palestina kutoka mji huo kwa mujibu wa mpango wa Jerusalem 2020.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |