• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa lalaani vikali shambulizi la bomu mjini Benghazi

    (GMT+08:00) 2019-08-11 16:56:18

    Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limefanya mkutano wa dharura kuhusu hali ya Libya na kulaani vikali shambulizi la bomu lililotegwa ndani ya gari katika mji wa Benghazi mashariki ya nchi hiyo, na kusisitiza kuwa Umoja wa Mataifa hautaondoka katika nchi hiyo.

    Wafanyakazi watatu wa Tume Maalumu ya Umoja wa Mataifa nchini Libya wameuawa kwenye shambulizi hilo, na wengine wengi wakiwemo wafanyakazi watatu wa Umoja wa Mataifa kujeruhiwa.

    Mwenyekiti wa zamu ya mwezi huu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambaye pia ni mwakilishi wa kudumu wa Poland katika Umoja huo Bi. Joanna Wronecka, ametoa salamu za rambirambi kwa jamaa za wahanga wa tukio hilo..

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako