Wizara ya utamaduni na utalii ya China imesema, katika nusu ya kwanza ya mwaka huu, matumizi ya kiutamaduni yametoa mchango mkubwa katika ongezeko la utalii nchini humo. Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na wizara hiyo, asilimia 80 ya watu wanaridhika na matumizi yao ya kiutamaduni. Lakini ripoti pia inasema, bado kuna nafasi nyingi za kufanyiwa maboresho kutokana na mawasiliano ya usafiri na migahawa karibu na maeneo ya kiutamaduni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |