• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kimbunga Lekima chasababisha vifo vya watu 45 na wengine 16 kutojulikana walipo nchini China.

    (GMT+08:00) 2019-08-12 20:06:27

    Kimbunga Lekima kimesababisha vifo vya watu 45 na wengine 16 kutojulikana walipo katika mikoa mitatu nchini China.

    Hadi Jumatatu asubuhi, idadi ya vifo vilivyotokana na kimbunga hicho mkoani Zhejiang imeongezeka hadi 39, wakati watu 9 bado hawajulikani walipo. Kimbunga hicho kimewaathiri wakazi milioni 6.68 mkoani humo, miongoni mwao milioni 1.26 wamehamishwa. Kimbunga hicho pia kimeharibu hekta laki 2.34 za mazao ya kilimo, na kusababisha hasara ya kiuchumi ya moja kwa moja ya dola bilioni 3.4 za kimarekani.

    Mbali na hayo, kimbunga hicho pia kimesababisha vifo vya watu watano mkoani Shandong na kifo cha mtu mmoja katika mkoa wa jiran wa Anhui.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako