• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mashabiki wamkataa Neymar PSG

    (GMT+08:00) 2019-08-13 10:08:26

    Mashabiki wa Paris Saint-German (PSG) wamemtolea uvivu mshambuliaji Neymar katika mechi ya ufunguzi wa Ligi Kuu Ufaransa iliyochezwa jumapili usiku. Licha ya kupata ushindi wa mabao 3 – 0 dhidi ya Nimes, mashabiki wa PSG walikwenda uwanjani na mabango ya kumtaka Neymar kuondoka kwenye klabu hiyo. Neymar ameibua mzozo wa muda mrefu na klabu yake akishinikiza kuondoka katika usajili wa majira ya kiangazi. Miamba ya soka Barcelona Hispania na Real Madrid inahusishwa na mpango wa kumsajili nahodha huyo wa zamani wa Brazil.
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako