Kampuni inayojishughulisha na mazoezi ya kisasa ya Bodystreet ya Ujerumani imetoa ofa ya masomo kwa mwaka mmoja kwa mchezaji bora wa timu ya Taifa ya Tanzania kwa wanawake chini ya miaka 20 (Tanzanite) Bi. Enekia Kasonga kusoma na kucheza mpira nchini humo. Ofa hiyo imetolewa wakati kampuni hiyo ikifungua tawi lake jijini Dar es Salaam, Tanzania.