Kenya imeipita Denmark, Fiji na Jamaica baada ya kushirikia michuano ya kombe la dunia jijini Johannesburg Afrika Kusini ilikoilipua Madagascar kwa miguso 35-5 na Uganda 37-5 kabla ya kuzidiwa ujanja na wenyeji Afrika Kusini kwa miguso 39-0 kwenye fainali iliyopigwa mwishoni mwa wikiendi.
Vimwana hao wanaofundishwa na kocha Oloo, ambao sasa watalazimika kushinda mchujo wa dunia utakaoleta pamoja timu kutoka Amerika Kusini, Ulaya, Asia na Oceania mwaka 2020 ili kuingia Kombe la dunia mwaka 2021 nchini New Zealand, wameimarisha alama zao kutoka 46.46 hadi 46.72 kwenye viwango hivyo vya mataifa 55.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |