Baada ya kupoteza mechi nne za kwanza, timu ya Chui ya Kenya ilifufua matumaini baada ya kuichapa Namibia 3-1 uwanja wa chuo kikuu cha Stellenbosch mjini Cape Town Afrika kusini.
Upande wa timu ya wanawake maarufu kama Tausi imeibuka ya nne kwa kujizolea alama nne baada ya kushinda mchezo mmoja, kutoka sare mara moja na kukubali vichapo mara tatu. Timu za Afrika Kusini (wanaume na wanawake) ziliendeleza ubabe wazo na kutwaa tiketi ya kushiriki Olimpiki za Tokyo mwaka 2020
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |