• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mashindano ya Afrika (All Africa Games 2019) yarindima Rabat

    (GMT+08:00) 2019-08-21 08:13:35
    Mashindano ya Afrika yajulikanayo zaidi kama All Africa Games yanaendelea jijini Rabat nchini Morocco. Zaidi ya wanamichezo 6,000 kutoka mataifa yote 54 ya Afrika wamekusanyika kushindana aina 30 za michezo inayojumuisha fani 17 zitakazotumika kama mashindano ya kufuzu Olimpiki.

    Ugunguzi wa mashindano hayo ulifanyika juzi na kuhudhuriwa na mwanamama Nawal El Moutawakel aliyekuwa mwanariadha wa kwanza mwanamke kutoka Afrika kushinda medali ya dhahabu ya Olimpiki katika mbio za mita 400 kuruka viunzi katika mashindano ya Olimpiki yam waka 1984.

    Naye mwanariadha wa zamani wa Kenya ambaye sasa ni afisa wa kamati ya Olimpiki ya Afrika Tegla Loroupe amesema mashindano ya All Africa Games ni kigezo cha wanariadha kujipima uwezo wao kushiriki mashindano ya Olimpiki.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako