Waziri mkuu wa Uingereza Bw. Boris Johnson ambaye yupo ziarani nchini Uingereza, amefanya mazungumzo na rais Emmanuel Macron wa Ufaransa, ajenda kuu ikiwa ni suala la mpaka wa Ireland lililopo kwenye Mpango wa Uingereza wa kujitoa kutoka Umoja wa Ulaya, Brexit.
Bw. Johnson amesema, ni lazima Uingereza ijitoe kwenye Umoja wa Ulaya Oktoba 31 bila ya kujali kama makubaliano yatafikiwa au la. Pia anatumai makubaliano yatafikiwa, na anatiwa moyo na mazungumzo kati yake na chansela wa Ujerumani Angela Merkel yaliyofanyika Jumatano huko Berlin.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |