Baraza la Serikali la China leo limewasilisha bungeni ripoti kuhusu hali ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya uchumi na jamii tangu mwaka huu uanze.
Ikizungumzia kazi za uchumi za nusu ya pili ya mwaka huu, ripoti hiyo imeeleza kuwa ni kipaumbele kuhakikisha utulivu na kushughulikia hatari katika kujiendeleza. Pia imetoa maagizo ya kushikilia maendeleo ya ngazi ya juu, kuharakisha mageuzi na uvumbuzi ili kuhamasisha nguvu za uhai za wahusika wakuu wa soko, kuhimiza uwazi wa hali ya juu na kupanua maeneo yanayofanyiwa ushirikiano wa kunufaishana kwa pande zote.
Wakati huohuo, mkurugenzi wa kamati ya maendeleo na mageuzi ya taifa ya China Bw. He Lifeng amesisitiza umuhimu wa kuvutia uwekezaji wa kigeni, kupanua soko la ndani lenye nguvu na kutafuta nguvu za matumizi katika sehemu za vijijini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |