Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limesema, wakimbizi 1,350 wamehamishwa salama Libya na kwenda katika nchi nyingine mwaka huu. Kutokana na ukosefu wa usalama na vurugu, Libya imekuwa sehemu inayopendelewa kutumiwa na wahamiaji haramu wanaotaka kuvuka bahari ya Mediterranean na kufika Ulaya, wengi wao wakifa maji njiani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |