• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Benki ya Standard Chartered ya Kenya inapanga kushirikiana na makampuni ya fedha ya China kuongeza mapato

    (GMT+08:00) 2019-08-26 20:00:38
    Benki ya Standard Chartered ya Kenya imetangaza kuwa inatafuta ushirikiano na makampuni ya teknolojia ya fedha ya China ili kuongeza mapato yake.

    Ofisa mkuu wa Benki hiyo Bw. Kariuki Ngari amesema mjini Nairobi kuwa kutokana na kuimarika kwa uwekezaji na biashara kati ya China na Kenya, wateja wa benki hiyo wanaangalia njia za kuweza kufanya malipo ya kuvuka mpaka. Amesema kutokana na mahitaji ya wateja, wanaweza kuunganisha majukwaa ya malipo kwa njia ya mtandao kama vile Alipay na WeChat, ili kurahisisha malipo kwenye biashara kati ya China na Kenya.

    Bw. Ngari amesema jumuiya ya wafanyabiashara wa China kwa sasa inatoa mchango mkubwa kwenye uchumi wa Kenya, na Benki ya Standard Chartered imeanzisha dawati la China kwenye matawi yake ili kuhudumia wateja wake wa China.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako