Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema, sharti la kwanza la kuanzisha tena mazungumzo kati yake na Marekani ni kwamba Marekani lazima irejee kwenye makubaliano ya nyuklia ya Iran JCPOA na mazungumzo hayo yanatakiwa kufanyika chini ya mfumo wa makubaliano hayo.
Rais Rouhani amefafanua kuwa Marekani pia lazima ijirekebishe makosa yake na kukubali haki halali ya Iran. Amesisitiza kuwa, mwelekeo wa suala hilo kwa sasa unategemea msimamo wa Marekani, kama Marekani haitaondoa vikwazo dhidi ya Iran, uhusiano kati ya nchi hizo mbili hautakuwa na maendeleo mazuri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |