Wizara ya afya ya Uganda imezindua kampeni ya miezi mitatu ya kuchangia damu kufuatia ongezeko la ukosefu wa damu lililosababishwa na ongezeko la ugonjwa wa malaria nchini humo. Akiongea katika shughuli za uzinduzi, waziri wa nchi anayeshughulika na huduma za afya Bibi Joyce Moriku Kaducu amesema kampeni hiyo inalenga kuongeza vitengo vya damu hadi elfu 50 kabla ya mwezi Novemba kutoka vitengo elfu 25 vya damu vya sasa. Pia amehamasisha wananchi kuchangia damu ili kuokoa maisha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |