Mwanasayansi wa China Tu Youyou aliyepewa tuzo ya Nobel mwaka 2015 kutokana na mchango wake wa kugundua dawa ya artemisinin yenye ufanisi wa kupambana na malaria, ameteuliwa kugombea medali ya Jamhuri ya China ambayo ni heshima ya juu zaidi nchini China. Bibi Tu mwenye umri wa miaka 89 amejishughulisha na utafiti wa matibabu ili kutafuta njia ya kutibu ugonjwa wa malaria na kuwaokoa mamilioni ya watu. Watu wengine 7 akiwemo Yuan Longping ambaye ni mtaalam wa kilimo na kujulikana kama "baba wa mpunga chotara" pia wameteuliwa kugombea medali hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |