• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais Kagame asema sekta binafsi inachangia ukuaji na maendeleo ya nchi

    (GMT+08:00) 2019-08-29 19:50:23
    Rais wa Rwanda Paul kagame jana aliwaambia viongozi wa dunia waliojumuika jijini Tokyo,Japan,kuweka sekta binafsi katika mkakati wa mafanikio na maendeleo.

    Aliyasema hayo jana katika mkutano wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD) ,ambao alisema ni mchakato mzuri unaowakilisha nia ya matumaini na ushirkiano.

    Alisema uvumbuzi wa TICAD umekuwa wastani na kwamba mkutano huo umeendelea kukua sanjari na vipaumbele vya Afrika.

    Aliongeza kuwa mabadiliko makubwa ni umuhimu uliopatiwa sekta binafsi katika mkutano huo wa TICAD.

    Aidha Rais Kagame aliitaja Rwanda kama mfano bora wa mafanikio wakati maendeleo ya sekta binafsi yanapowekwa katika mkakati wa ustawi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako