• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Jamii ya wafanyabiashara wa Uingereza yawa na wasiwasi juu ya uamuzi wa waziri mkuu kusimamisha bunge

    (GMT+08:00) 2019-08-30 08:43:38

    Jamii ya wafanyabiashara wa Uingereza jana imeendelea kuwa na wasiwasi juu ya mgogoro wa kisiasa huku vita vya maneno juu ya uamuzi wa waziri mkuu Boris Johnson wa kusimamisha bunge la Uingereza vikizidi kupamba moto.

    Mkurugenzi Mkuu wa shirikisho la wafanya biashara BCC Adama Marshal amesema biashara nchini Uingereza imekuwa kwenye mchezo usiokwisha wa chesi ya kisiasa, wakati biashara kadhaa na hali ya uchumi ya Uingereza ikiwa hatarini.

    Johnson amepata idhini kutoka kwa Malkia Elizabeth ya kusimamisha bunge, au kuahirisha kwa karibu wiki tano katika mwezi Septemba na Oktoba. Wakosoaji wanasema hatua hiyo inaaminiwa kuwa ni jaribio la Johnson kupunguza nafasi za wabunge kupitisha sheria za kuzuia Brexit bila ya makubaliano.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako