Katika droo hiyo iliyofanyika sambamba na tuzo za mwanasoka bora wa Ulaya, Mbwana Samatta amejikuta timu yake ya KRC Genk ikipangwa kundi moja na Liverpool ambapo Sadio Mane raia wa Senegal watakutana kwa mara nyingine.
Mane aliiongoza Senegal kuichapa Tanzania ya Samatta 2-0 kwenye mechi ya Kundi C fainali za kombe la mataifa ya Afrika Juni mwaka huu nchini Misri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |